(a) Vitenzi vya kigeni
Katika Sarufi ya Kiswahili, kuna vitenzi vya kigeni ambavyo hutumiwa katika uundaji wa nomino. Kwa mfano:
| Kitenzi cha Kigeni | Nomino Inayovyazwa |
| Fahamu | Ufahamu |
| Safiri | Safari, Msafiri, Usafiri |
| Sahau | Usahaulivu |
| Samehe | Usamehevu, Msamaha, Msamehevu |
| Afiki | (Ma)afikiano |
| Ahidi | Ahadi |
(b) Vitenzi vya kuambisha viambishi
Nomino mbalimbali huundwa kwa kuambisha viambishi katika vitenzi kama ilivyo hapa chini:
(a) Kiambishi awali ‘m‘
Kiambishi hiki huambishwa ili kuonyesha mtendaji
Mifano:
| Kitenzi | Nomino |
| Safiri | Msafiri |
| Hakiki | Mhakiki |
| Rithi | Mrithi |
| Zuka | Mzushi |
| Sajili | Msajili |
(b) Kiambishi tamati ‘o’
Kiambishi hiki huambishwa kuonyesha tokeo la kitendo.
Mifano:
| Kitenzi | Nomino |
| Jaribu | Jaribio |
| Tisha | Tisho |
| Funza | Funzo |
| Lenga | Lengo |
| Nena | Neno |
(c) Kiambishi awali ‘ki’
Kiambishi hiki kinapoambishwa huonyesha kitu kilichotumika
kufanyia tendo.
Mifano:
| Kitenzi | Nomino |
| ziba | kizibo |
| chunga | kichungio |
| bana | kibanio |
(d) Kiambishi tamati ‘ji’
Kiambishi hiki kinapoambishwa huonyesha hali ya mazoea ya mtendaji.
Mifano:
| Kitenzi | Nomino |
| Chora | Mchoraji |
| Saka | Msakaji |
| Fuga | Mfugaji |
(e) Kiambishi awali ‘ku’
Kiambishi hiki huambishwa ili kuonyesha kitenzi-jina kutokana na
kitenzi hicho.
Mifano:
| Kitenzi | Nomino |
| Fadhili | Kufadhili |
| Ghilibu | Kughilibu |
| Soma | Kusoma |
(f) Kiambishi ‘u’ awali
Kiambishi hiki huambishwa ili kuonyesha udhahania.
Udhahania ni kinyume na uhalisi; ni fikra, hali ya kufikiria jambo lisilogusika wala kuonekana.
Mifano:
| Kitenzi | Nomino |
| Ogopa | Uoga |
| Tafiti | Utafiti |
| Teua | Uteuzi |
| Funza | Ufunzaji |
| Choka | Uchovu |
(g) Kiambishi tamati ‘i’
Kiambishi hiki kikiambishwa kwenye kitenzi huonyesha mtendaji na udhahania.
Mifano:
| Kitenzi | Mtendaji | Udhahania |
| Lea | Mlezi | Ulezi |
| Asi | Mwasi | Uasi |
| Pika | Mpishi | Upishi |
Kama inavyodhihirika hapo juu, inawezekana kuunda nomino kutokana na vitenzi. Nomino zilizoundwa huwa na maana maalum kutegemea kiambishi kilichoambishwa.