UUNDAJI WA NOMINO KUTOKANA NA VITENZI: KIGENI, KUAMBISHA VIAMBISHI

(a) Vitenzi vya kigeni

Katika Sarufi ya Kiswahili, kuna vitenzi vya kigeni ambavyo hutumiwa katika uundaji wa nomino. Kwa mfano:

Kitenzi cha KigeniNomino Inayovyazwa
FahamuUfahamu
SafiriSafari, Msafiri, Usafiri
SahauUsahaulivu
SameheUsamehevu, Msamaha, Msamehevu
Afiki(Ma)afikiano
AhidiAhadi

(b) Vitenzi vya kuambisha viambishi

Nomino mbalimbali huundwa kwa kuambisha viambishi katika vitenzi kama ilivyo hapa chini:

(a) Kiambishi awali ‘m

Kiambishi hiki huambishwa ili kuonyesha mtendaji

Mifano:

KitenziNomino
SafiriMsafiri
HakikiMhakiki
RithiMrithi
ZukaMzushi
SajiliMsajili

(b) Kiambishi tamati ‘o’

Kiambishi hiki huambishwa kuonyesha tokeo la kitendo.

Mifano:

KitenziNomino
JaribuJaribio
TishaTisho
FunzaFunzo
LengaLengo
NenaNeno

(c) Kiambishi awali ‘ki’

Kiambishi hiki kinapoambishwa huonyesha kitu kilichotumika

kufanyia tendo.

Mifano:

KitenziNomino
zibakizibo
chungakichungio
banakibanio

 (d) Kiambishi tamati ‘ji’

Kiambishi hiki kinapoambishwa huonyesha hali ya mazoea ya mtendaji.

Mifano:

KitenziNomino
ChoraMchoraji
SakaMsakaji
FugaMfugaji

 (e) Kiambishi awali ‘ku’

Kiambishi hiki huambishwa ili kuonyesha kitenzi-jina kutokana na

kitenzi hicho.

Mifano:

KitenziNomino
FadhiliKufadhili
GhilibuKughilibu
SomaKusoma

 (f) Kiambishi ‘u’ awali

Kiambishi hiki huambishwa ili kuonyesha udhahania.

Udhahania ni kinyume na uhalisi; ni fikra, hali ya kufikiria jambo lisilogusika wala kuonekana.

Mifano:

KitenziNomino
OgopaUoga
TafitiUtafiti
TeuaUteuzi
FunzaUfunzaji
ChokaUchovu

 (g) Kiambishi tamati ‘i’

Kiambishi hiki kikiambishwa kwenye kitenzi huonyesha mtendaji na udhahania.

Mifano:

KitenziMtendajiUdhahania
LeaMleziUlezi
AsiMwasiUasi
PikaMpishiUpishi

Kama inavyodhihirika hapo juu, inawezekana kuunda nomino kutokana na vitenzi. Nomino zilizoundwa huwa na maana maalum kutegemea kiambishi kilichoambishwa.

Tags: 3372

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *