Malumbano ya utani ni utanzu wa vichekesho katika fasihi simulizi. Jamii za Kiafrika zina tafrija mbalimbali zinazojumuisha furaha na vichekesho nyingi kama njia mojawapo ya burudani miongoni mwa wanajamii. Lakini katika vichekesho hivyo kuna mafunzo tele.