Hojaji ni mkusanyiko wa maswali ambayo hutumiwa kama kifaa katika kazi ya utafiti. Maswali haya hayatungwi kiholela bali hujifunga sana na mada na aina ya utafiti wa nyanjani unaohusika.
KUANDIKA: KUJAZA FOMU
Fomu ni aina ya maandishi yenye maagizo fulani na mapengo yanayohitaji kujazwa kwa ufupi na usahihi.