SARUFI: UPATANISHO WA KISARUFI: VIREJESHI ‘O’ NA ‘AMBA-

Virejeshi ni viambishi vinavyorejesha nomino kwa kitendo. Aidha, hutokea kabla au baada ya mzizi wa kitenzi ili kurejelea nomino ambayo habari yake inatolewa. Virejeshi huweza kutokea pia kwenye mzizi “amba-“.

Tazama jedwali lifuatalo:

NgeliNominoVirejeshi
AMwalimuambaye/aliyekuja ni Mchina.
WAWalimuambao/waliokuja ni Wachina.
UMtiambao/utakaopandwa ni mvule.
IMitiambayo/itakayopandwa ni mivule.
KIChakulaambacho/kitakachosazwa kitatupwa.
VIVyakulaambavyo/vitakavyosazwa vitatupwa.
LIYaiambalo/lililovunjika linanuka.
YAMayaiambayo/yaliyovunjika yananuka.
IBaruaambayo/uliyoniandikia iliniudhi.
ZIBaruaambazo/mlizotuandikia zilituudhi.
UUamuziambao/uliofanywa unaridhisha.
YAMaamuziambayo/yaliyofanywa yanaridhisha.
KUKuchezaambako/walikocheza kulifurahisha.
PAPahaliambapo/nilipotengewa panatosha.
KUKwahaliambako/kulikochafuka kutasafishwa.
MUMwahaliambamo/mnamonuka mtapulizwa marashi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *