SARUFI – NGELI ZA NOMINO: UPATANISHO WA KISARUFI NA VIVUMISHI VYA A-UNGANIFU

Kama ilivyoelezwa katika sehemu mbalimbali za Tanzu za Lugha, nomino inayotumika huathiri muundo wa viambishi vingi vinavyotokea katika maneno yaliyotumika. Lugha ya Kiswahili, kama lugha nyingine za Kibantu, ina utaratibu wa nomino ambapo muundo wa viambishi vya maneno (vitenzi, vivumishi, viwakilishi, vielezi na kadhalika) huongozwa na aina ya nomino. Kwa mfano:

  • Chebii alikuwa mwanamichezo aliyejulikana Afrika nzima.

Nomino ndiyo inayotawala sentensi nzima na huathiri viambishi vinavyohusiana nayo. Vivumishi vya A-Unganifu ni virai vinavyovumisha nomino.

Kwa mfano:

  • Suruali ya Moseti
  • Jina la Lokorito

Kama ilivyodokezwa hapo juu virai hivi hutegemea ngeli ya nomino.

Kwa mfano:

A: Mtoto wa mama

WA: Watoto wa mama

U: Mlima wa Kenya

I: Milima ya Kenya

U: Ugonjwa wa kifua

YA: Magonjwa ya kifua

LI: Jino la dhahabu

YA: Meno ya dhahabu

KI: Cheti cha uanasheria

VI: Vyeti vya uanasheria

I: Nyumba ya wazazi

ZI: Nyumba za wazazi

I: Hewa ya siku hizi

I: Hewa ya siku hizi

U: Ukuta wa mawe

ZI: Kuta za mawe

U: Ukarimu wa mwalimu

U: Ukarimu wa mwalimu

KU: Kusoma kwa kasi

PA: Pahali pa kupumzika

KU: Kwahali kwa kupumzika

MU: Mwahali mwa kupumzika

Kama inavyodhihirika hapo juu, A-Unganifu inashikamanisha nomino mbili na hubadilika kutegemea ngeli. Wanafunzi wengi husumbuliwa na upatanisho wa kisarufi ilhali ni sehemu muhimu sana ya lugha ya Kiswahili. Mwanafunzi anahimizwa ajitahidi kadri iwezekanavyo ili aimarishe sarufi yake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *