FASIHI: NYIMBO ZA TAARAB

Ufuatao ni mfano wa wimbo

wa taarab:

Nitakupa maarifa x4

Uketi ukiyaandika

Ashibaye hukinai x3

Hamjui mwenye njaa.

Nyimbo za taarabu

Nyimbo za taarab ni kielelezo bora cha ufanisi na uamilifu wa nyimbo miongoni mwa wanajamii wa mwambao wa Afrika Mashariki. ‘Taarab’ ni neno la Kiarabu lenye maana ya ‘furaha’. Ni muziki wa kustarehesha na kuwaburudisha watu wa matabaka yote. Hupoza machofu ya umma.

Aidha, ni aina moja ya fasihi simulizi inayotumika hasa katika sehemu za mwambao wa pwani ya Afrika Mashariki. Ni maarufu sana Mombasa na Unguja Inasemekana kwamba taarab ililetwa Afrika Mashariki mnamo mwanzoni mwa 1870. Kuna madai kuwa Sultan wa Unguja Seyyid Barghash, aliyependa anasa na starehe, aliwaalika watribu kutoka Misri waje kumtumbuiza. Wenyeji wakavutiwa na muziki huu na wakajifunza kupiga vyombo na kuimba. Vyama vingi vya taarab vimeundwa tangu siku hizo kama vile Lucky Star, Black Star, na Muungano, na waimbaji maarufu kama vile Siti Binti Saad na Shakila kujitokeza.

Taarab hutumia lugha yenye mvuto. Aghalabu hutumia mtindo wa kishairi Ushairi utumikao zaidi ni ule wenye urari wa vina na mizani. Lugha ya kishairi husababisha matumizi ya lugha ya kiishara na mafumbo.

Kwa mfano:

Nakuonya tahadhari punguza kulirandia Sega langu la asali najua walinyatia

Utakufika muhali vya watu kuvivamia

Walinzi wake wakali mashujaa walotimia

Hata tembo mwenye hali hathubutu kusogea

Walinzi wake ambao wakali wasochelea

Bunduki na marisao wameshinda kufyatua

Mikuki na zao ngao ni bure wamekimbia

Seuze we mwanakwao huna unachokililia

Umepigwa mpumbao mate unakimezea

Wameshindwa wenye vyao seuze wewe raia?

Kiitikio:

Hebu acha kujigamba huna unachokipata

Haiwi tembo na simba umewashinda ukuta.

Taarab, japo ni muziki wa starehe, si ngoma ya starehe tu. Inafanya kazi ya kuwaraghibisha wananchi kiitikadi. Wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere nchini Tanzania, kwa mfano, taarab ilitumiwa kuendeleza siasa ya Ujamaa. Ushairi huu hutoa mawaidha mema kwa wanajamii. Tazama taarab ifuatayo kuhusu ujana.

Ujana umenipoteya, kama moshi siuoni

Na nguvu zimenitoka, hazimo tena mwilini

Na sasa nimeshakuwa, nimeingia uzeeni

Shujaa nilikuwa ya kweli namwambieni

Na nguvu zilinijaa sikuhofu asilani

Na sasa nimeshikwa, sina raha duniani

Dunia ina hadaa hilo nimeliamini

Dunia ina fazaa sasa nimekuwa duni

Sasa nimeshachakaa, na ujana siuoni

Majuto yamenijaa sijui nifanye nini

Kwa mambo yalotokea, mimi kwenda uzeeni

Wala sikufikiria, hayakuja akilini

Kiitikio:

Uwapi ujana wangu, ule nikijivunia

Umepita kama moshi, mara umeshapotea.

ZOEZI

(a) Taarab ilizinduliwa vipi katika maeneo ya pwani ya Afrika Mashariki? (

b) Muziki wa taarab unatumiwa kwa shughuli gani za kijamii?

(c) Eleza maana ya:

(i) uamilifu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *